USIKOSE KUANGALIA MATOKEO YA MECHI ZA KIRAFIKI


 
Usiku wa kuamkia leo kumechezwa michezo ya kirafiki ya kimataifa ikiwa ni michezo ya kujiandaa na michuano ya kombe la ulaya.
Mabingwa wa kombe la dunia mwaka 2010 Hispania walitosha nguvu na itali kwa kufunga bao 1-1,Uturuki wakapata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Swedeni.
Malta wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani wameambulia sare ya 0-0 na Moldova, Norway na Estonia nao wakashindwa kutambiana baada ya kwenda sare ya bila bila.
Matokeo mengine
Ugiriki 2-1 Montenegro 1
Denmark 2 -1Iceland 1
Ukraine 1-0 Cyprus 0
Jamuhuri ya Czech 0-1 Scotland
wales 1-1 Ireland ya kaskazini
Michezo ya kufuzu Afcon kuendelea leo

Michezo ya kufuzu Afcon kuendelea leo

Kikosi cha Taifa la Ghana
Michezo ya kusaka tiketi ya kushiki michuano ya kombe la mataifa ya afrika mwaka 2017 itayofanyika Gabon itaendelea tena leo
Katika kundi A timu ya taifa ya Djibout itakua nyumbani katika uwanja wake wa Djibouty kukipiga na liberia.
Ghana maarufu kama the Black Stars walioko kundi H watakua wenyeji wa timu ya Mozambique wanaofahamika kama Mambas.
Comoros watashuka dimbani kuwakabili Botswana huku Madagascar akipimana ubavu na timu ya taifa ya Jamuhuri ya Africa ya kati.
 Ratiba ya Mechi za Klabu Bingwa Kimataifa

Ratiba ya Mechi za Klabu Bingwa Kimataifa


 Tokeo la picha la Ligi ya Premia
Msimu mpya wa Ligi ya Premia utaanza Jumamosi tarehe 13 Agosti.
Ratiba ya Mechi za Klabu Bingwa Kimataifa
  • 23 Julai - Celtic v Leicester, Glasgow
  • 24 Julai - Inter v PSG, Eugene
  • 27 Julai - Real Madrid v PSG, Columbus
  • 27 Julai - Bayern Munich v AC Milan, Chicago
  • 27 Julai - Chelsea v Liverpool, Pasadena
  • 30 Julai - Celtic v Barcelona, Dublin
  • 30 Julai - Inter v Bayern Munich, Charlotte
  • 30 Julai - AC Milan v Liverpool, Santa Clara
  • 30 Julai - PSG v Leicester, LA
  • 3 Agosti - Barcelona v Leicester, Stockholm
  • 3 Agosti - Bayern Munich v Real Madrid, East Rutherford
  • 3 Agosti - AC Milan v Chelsea, Minnapolis
  • (Kuthibitishwa baadaye) - Liverpool v Barcelona
  • (Kuthibitishwa baadaye) - Inter v Celtic
  • (Kuthibitishwa baadaye) - Real Madrid v Chelsea

TAIFA STARS YAICHAPA CHAD BAO 1-0


Mbwana Samatta akivaa kitambaa cha unahodha kwa mara ya kwanza, amekiongoza kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kupata ushindi wa goli 1-0 ugenini dhidi ya Chad kwenye mchezo wa Group G kuwania nafasi ya kushiriki michuano ya kombe la mataifa ya Afrika inayotarajiwa kufanyika mwaka 2017 nchini Gabon.

Mbwana Samatta amefunga goli hil kipindi cha kwanza akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Farid Musa goli ambalo limedumu hadi dakika 90 za mchezo huo.

Stars imefikisha pointi 4 baada ya kucheza michezo 3, matokeo hayo yanaifanya Stars ifikishe idadi sawa ya pointi na Nigeria ‘The Super Eagles’ lakini Stars ipo mbele ya Nigeria kwa mchezo mmoja. Nigeria itakutana na Misri kwenye mchezo wa kundi ilo siku ya Ijumaa.

Stars itacheza mchezo wake wa marudiano dhidi ya Chad siku ya Jumatatu March 28 mwaka huu kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam.

Msimamo wa Group G unaongowa na Misri yenye pointi 6 ikifatiwa na Nigeria na Tanzania zenye pointi 4 lakini Nigeria ikishika nafasi ya pili kwa tofauti ya magoli wakati Chad ikiwa ya mwisho bila pointi. Tanzania na Chad zimecheza mechi 3 mechu moja mbelea ya Misri na Nigeria.

Matokeo ya mechi nyingine za kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa mechi ambazo tayari zimemalizika yapo kama ifuatavyo:

Guinea-Bissau 1-0 Kenya

South Sudan 1-2 Beni
kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani iliyotwaa kombe la dunia Franz Beckenbauer ametajwa katika orodha ya watuhumiwa 6 wanaoshukiwa kutoa hongo kununua kombe la dunia la mwaka wa 2006

kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani iliyotwaa kombe la dunia Franz Beckenbauer ametajwa katika orodha ya watuhumiwa 6 wanaoshukiwa kutoa hongo kununua kombe la dunia la mwaka wa 2006

 
Beckenbauer na wengine 5 kuchungwa na FIFA
Aliyekuwa Nahodha na kisha kocha wa timu ya taifa ya Ujerumani iliyotwaa kombe la dunia Franz Beckenbauer ametajwa katika orodha ya watuhumiwa 6 wanaoshukiwa kutoa hongo kununua kombe la dunia la mwaka wa 2006 huko Ujerumani.
Kamati ya maadili ya FIFA imetoa orodha wa watu 6 waliongoza kampeini hiyo ya kutwaa uwenyeji wa kombe la dunia.
Shirikisho la soka la Ujerumani lilipasua mbarika lilipofichua ripoti ya upelelezi ambayo ilimpelekea Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya Ujerumani kukiri kuwa alifanya makosa wakati wa kuwania zabuni ya wenyeji wa kombe hilo la dunia.
Mnamo mwezi Oktoba mwaka uliopita, Beckenbauer, 70, aliomba msamaha kwa hatua na kauli alizotoa wakati wa kuwania uwenyeji wa mashindano hayo.
Ujerumani wakati huo iliishinda Afrika Kusini kwa kura moja pekee.
 
Mnamo mwezi Oktoba mwaka uliopita, Beckenbauer, 70, aliomba msamaha kwa hatua na kauli alizotoa wakati wa kuwania uwenyeji wa mashindano hayo.
Ujerumani ilipata kura 12 dhidi ya 11 za Afrika Kusini katika uchaguzi uliofanyika mwaka wa 2000.
Orodha kamili
  1. Franz Beckenbauer
  2. Wolfgang Niersbach
  3. Helmut Sandrock
  4. Theo Zwanziger
  5. Horst Schmidt
  6. Stefan Hans
 
Beckenbauer aliiongoza kikosi cha taifa cha West Germany wakati huo kutwaa kombe la dunia la mwaka wa 1974.
Jarida la upekuzi la Ujerumani, Der Spiegel mwaka uliopita liliripoti kuwa waandalizi wa kombe hilo walitenga Euro milioni 6.7 kununua uwenyeji wa mashindano hayo.
Beckenbauer, Zwanziger, Schmidt na Hans awanachunguzwa kwa makosa ya kutoa hongo ilikuwashawishi wajumbe waipigie Ujerumani kura pamoja na kutoa zabuni kadhaa kwa wajumbe fulani.
Kwa upande wao Niersbach na Sandrock wanachunguzwa kwa kosa la kushindwa kuripoti ukiukwaji wa kanuni na maadili ya FIFA.
Beckenbauer aliiongoza kikosi cha taifa cha West Germany wakati huo kutwaa kombe la dunia la mwaka wa 1974.
Aidha aliifunza timu hiyo miaka 16 baadaye ilipoibuka mabingwa wa dunia nchini Italia.
Amewahi pia kuifunza timu za Marseille na Bayern Munich, ambako anaihumia kama rais.
Tanzania,Kenya uwanjani kombe la mataifa Afrika

Tanzania,Kenya uwanjani kombe la mataifa Afrika

Taifa Stars ya Tanzania imesafiri Chad kwa mechi ya kundi ya la G
Kenya, Tanzania na Sudan Kusini zitakuwa uwanjani hapo kesho kutafuta tiketi ya safari ya Gabon mwakani kwa mashindano ya kombe la mataifa ya Afrika..
Kenya iko ugenini dhidi ya Guinea Bissau kundi E, Tanzania imesafiri Chad kwa mechi ya kundi ya la G huku Sudan Kusini ikiikaribisha ikiikaribisha Benin mechi ya kundi C..
Mechi zingine zitakazochezwa kesho ni Sao Tome wako nyumbani dhidi ya Libya kundi F na Zambia wanakaribisha Congo kundi E, na kesho kutwa mechi ya kundi la B, Madagascar inapambana nyumbani na Afrika ya Kati..
Harambee Stars ya Kenya itakuwa na wachezaji wake wa kutegemewa wa ng'ambo wakiongozwa na kiungo mkabaji wa Southampton Victor Wanyama, kipa Arnold Origi na Michael Olunga.
 
Nahodha wa Kenya Victor Wanyama
Baada ya kucheza mechi mbili Kenya ni ya tatu na pointi moja tu, Congo ikiwa juu na pointi nne ikifuatiwa na Congo na Zambia..
Nahodha mpya wa Taifa Stars ya Tanzania Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ni tegemeo kubwa kwenye mechi yao na Chad.
Taifa Stars ni ya tatu kundi G na pointi moja tu kwa mechi mbili walizocheza, kwanza wakameza mabao matatu bila jibu kisha wakaenda sare na Super Eagles ya Nigeria.
Misri inaongoza kundi hilo na pointi sita, Nigeria ya pili na nne..
 
Alex Iwobi wa Arsenal na Nigeria
Nigeria kwa sasa inaomba na kuamini kuwa nyota wa Arsenal Alex Iwobi atapata afueni na kuiwakilisha taifa hilo Super Eagles ya Nigeria itakapochuana na Firauni..
Sudan Kusini inashikilia nafasi ya pili kundi C na pointi tatu huku Mali ikiwa juu na nne, Benin ya tatu na Equatorial Guinea ya mwisho..
Mechi za marudiano zitachezwa wikendi hii kwa wanaocheza leo...
Mkurugenzi mkuu wa maandalizi ya michuano ya tenisi huko Indian Wells Raymond Moore amejiuzulu baada ya matamshi yake

Mkurugenzi mkuu wa maandalizi ya michuano ya tenisi huko Indian Wells Raymond Moore amejiuzulu baada ya matamshi yake

 
Raymond Moore
Mkurugenzi mkuu wa maandalizi ya michuano ya tenisi huko Indian Wells Raymond Moore amejiuzulu baada ya matamshi yake yaliozua utata kuhusu wanawake katika mchezo huo.
Moore mwenye umri wa miaka 69,amesema kuwa mchezo wa tenisi wa wanawake unategemea sana wanaume,maoni yalioelezewa kuwa ya ubaguzi wa jinsia na muungano wa tenisi nchini Marekani USTA.
Mchezaji nambari moja duniani kwa upande wa wanawake Serena Williams alisema kuwa matamshi ya Moore yana kera na yasio ya ukweli.
Lakini mwenzake kwa upande wa wanaume Novak Djokovic alidai kuwa ziara yake inafaa kupigania wanaume wapewe fedha zaidi.
 
Serana Williams
Moore alisema kuwa wachezaji wanawake wanafaa kuwapigia magoti wenzao wa kiume kama vile Roger Federer na Rafael Nadal.
Lakini mchezaji huyo wa zamani wa Afrika Kusini baadaye aliomba msamaha kwa matamshi yake.
Gwiji wa mchezo huo Martina Navratilova alisema kwamba matamshi ya Moore yanachukiza sana,akiongezea kuwa wachezaji wanawake huenda wakasusia michuano ya Indian Wells iwapo Moore ataendelea kuwa mwandalizi.
 
Novak Djokovic
Djokovic ambaye alishinda taji la BNP la Paribas Open huko India Wells siku ya Jumapili aliyaelezea matamshi ya Moore kama yasio sawa.
Lakini raia huyo wa Serbia mwenye umri wa miaka 28 alihoji kwamba wanaume wanafaa kupewa fedha zaidi kwa sababu watu wengi huangalia mechi zao.
Cech mchezaji bora wa mwaka

Cech mchezaji bora wa mwaka

 
Mchezaji bora nchini Czech Peter Cech
Golikipa wa kimataifa ya Jamuhuri ya Czech Petr Cech ametangazwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa nchi hiyo.
Cech Mwenye umri wa miaka 33,alichaguliwa na makocha, wachezaji na viongozi wa timu kutwaa tuzo ya nane ya uchezaji bora nchini mwake.
Golikipa huyu amewazidi wachezaji wenzake wa timu ya taifa Mshambuliaji wa Sparta Prague David Lafata, na kiungo wa Vladimir Darida anayeichezea Hertha Berlin.
kipa huyu wa klabu ya Soka ya Arsenal ameichezea timu ya taifa michezo 118 tangu alipoanza soka la kimataifa mwaka 2002.
Taifa Stars ya Tanzania Uso kwa Uso na Chad

Taifa Stars ya Tanzania Uso kwa Uso na Chad

 
Taifa Stars ya Tanzania kuchuana na Chad Jumatano
Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars itashuka dimbani hapo kesho, huko nchi Chad katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2017.
Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 11 kwa saa za nyumbani Afrika Mashariki.
Taifa Stars, imefanya mazoezi ya mwisho kuelekea mchezo huo katika uwanja wa Omnisports Idriss Mahamat Ouya ulipo katika jiji la D'jamena.
Kocha anayekinoa kikosi hicho Charles Boniface Mkwasa amesema anashukuru vijana wake hakuna majeruhi na wote wameweza kufanya mazoezi aliyoyapangilia.
Alex Iwobi: England na Nigeria zamng'ang'ania

Alex Iwobi: England na Nigeria zamng'ang'ania

 
Alex Iwobi
England iko mbioni kumzuia nyota wa Arsenal Alex Iwobi asijiunge na timu ya Super Eagles ya Nigeria.
Hii inafwatia kauli ya chipukizi huyo ya kuasi timu ya taifa ya Uingereza na badala yake kujiunga na vigogo wa soka ya Afrika Super Eagles ya Nigeria.
Iwobi ameshajumuishwa katika kikosi cha Nigeria kinachoratibiwa kuchuana dhidi ya Misri siku ya Ijumaa 26 -29 Machi katika mechi ya kufuzu kwa kombe la mataifa ya Afrika.
England imeanza harakati za kumshawishi asijiunge na Nigeria kwani hilo litawanyima fursa ya kumshirikisha katika timu ya taifa ya England.
Iwobi mwenye umri wa miaka 19 aliichezea England katika mashindano ya dunia ya vijana wasiozidi umri wa miaka 16,17 na hata 18 kabla ya kuamua kuwa angependa kuiwakilisha taifa alikozaliwa yaani Nigeria kuambatana na kanuni za FIFA.
Jarida la Daily Mirror linaripoti kuwa harakati za kimya kimya zinafanywa ilikumshawishi Iwobi abadilishe kauli yake kabla ya Ijumaa, kwani akishaichezea Super Eagles itakuwa vigumu mno kuichezea England katika mechi za kimataifa.
Iwobi amejumuishwa katika timu ya kwanza ya klabu yake ya Arsenal.

Kategori

Kategori